Muasisi na Mwenyekiti wa Bodi wa Precision Air Bw.
Michael Shirima akizungumza na hadhara ya abiria wa kwanza wa safari ya
Precision Air kwenda Johannesburg katika kumbi ya VIP uwanja wa
kimataifa
Julius Nyerere. Bw. Shirima alitumia nafasi hiyo kuwashukuru wateja na
wadau
wote wa Precision Air kwa ushirikiano mkubwa walionyesha kuweza
kufanikisha safari
hizo. “Hakika hii ni hatua kubwa sana lakini najua bila nyinyi
tusingeweza
kufika hapa, kwahiyo napenda kuwapongeza wateja wetu na wafanyakazi wote
wa
Precision Air kwa kazi nzuri. Nategemea mtafaidika kibiashara na kitalii
kwa safari hizi,” alisema. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu na Meneja
Mwendeshaji wa Precision Air Bw. Alfonse Kioko na Mkurugenzi wa Mamlaka
ya Anga
nchini Tanzania (TCAA) Bw. John Njawa.
Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini Mh. Radhia Msuya (katikati) alikuwepo kupokea ujumbe kutoka Precision Air jijini Johannesburg katika uwanja wa ndege wa kimataifa Oliver Tambo. Kushoto kwake
ni Mkurugenzi Mkuu na Meneja Mwendeshaji wa Precision Air Bw. Alfonse
Kioko na Dr. William Nshama. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya
Anga
nchini Tanzania (TCAA) Bw. John Njawa na Mkurugenzi wa Biashara wa
Precision Air Bw. Phil Mwakitawa. Balozi Msuya alifanya mahojiano na
waandishi wwa habari na alisema kwamba Precision Air sasa ni kiungo
muhimu katika kuendeleza uhusiano mzuri baina ya nchi hizo mbili hasa
hasa katika utalii na biashara.
Abiria wa safari namba PW 700 Kusini wakielekea kupanda
ndege tayari kwa kupasua anga kwenda Johannesburg Afrika.
Ndege aina ya Boeing 737-300 ikijitaharisha kuondoka
uwanja wa ndege wa kimataifa Julius Nyerere jijini Dare es Salaam. Ndege hiyo
iliondoka saa 2 na dakika 20 usiku.
Hi ndivyo hali ilivyokuwa ndani ya ndege hiyo
iliyofanya safari ya masaa 4 kwenda Johannesburg, ilibeba ya abiria 111, jumla ndege
hiyo inauwezo wakubeba abiria 116.
Wadau wa Precision Air wakifurahia huduma za Business
Class kwenda Johannesburg nchini Afrika Kusini ndani ya Boeing 737-300.
Mdau Amani Nkurlu Afisa Mawasiliano wa Precision Air
akiwa na mwanahabari mkongwe Jenerali
Ulimwengu katika hafla fupi ya mapokezi yaliyofanyika katika uwanja wa ndege wa
kimataifa wa Oliver Tambo, Johannesburg nchini Afrika Kusini. Msafara maalumu
wa Precision Air ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu na Meneja Mwendeshaji wa
Precision Air Bw. Alfonse Kioko upo Jo’Burg nchini Afrika Kusini kwa uzinduzi
na ziara maalumu itakayochukua takribani ya siku mbili.
Bw. Robert Kahendaguza (kulia) na Jumanne Fhika, wote
maafisa Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini wakiwa na mwanahabari mkongwe Jenerali
Ulimwengu katika tafrija ya mapokezi ya Precision Air iliyofanyika uwanja wa
ndege wa kimataifa O. Tambo jijini Jo’Burg.
Wadau mbali mbali wenyeji wa Afrika Kusini na
Tanzania wote walihudhuria hafla hiyo katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa O.
Tambo.









No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)