Katibu
Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo akipata maelezo ikiwa
ni pamoja na kuoneshwa juu ya shughuli za upimaji wa mafuta ya magari
unavyofanywa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji
(EWURA) alipotembelea banda hilo kwenye maonesho hayo.Anayetoa maelezo
ni Mhandisi Melania Kamugisha ambaye ni mtaalamu wa mamlaka hiyo.
Naibu
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai (CCM)
akipata maelezo kutoka kwa mtaalamu wa mradi wa Biofueli, Ester Mfugale
alipotembelea jana banda la Wizara ya Nishati na Madini kwenye maonesho
yake yanayoendelea kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma.
Naibu
Waziri wa Fedha na Uchumi, Gregory Teu, akipata maelezo kutoka kwa
mtaalamu kutoka Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Assa Mwakilembe
juu ya shughuli zinazofanywa na Wizara hiyo mara alipotembelea banda
hilo jana.
Naibu
Waziri wa Fedha na Uchumi, Gregory Teu, akipata maelezo kutoka kwa
mtaalamu kutoka kampuni ya Arti Tanzania Limited inayofadhiliwa na
Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Abdalah Seushi juu ya shughuli
zinazofanywa na kampuni hiyo mara alipotembelea banda hilo kwenye
maonesho ya Wizara ya Nishati na Madini yanayoendelea katika viwanja
vya Bunge mjini Dodoma.
Waziri
Kivuli wa Wizara ya Nishati na Madini, Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John
Mnyika (CHADEMA) akimsikiliza kwa makini Mtendaji Mkuu wa Wakala wa
Ukaguzi wa Madini Nchini (TMAA),Paul Masanja alipotembelea banda hilo
ili kupata maelezo juu ya shughuli za ukaguzi wa madini zinazofanywa na
Wakala huo.Picha Zote na Mdau Greyson Mwase





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)