RAIS KIKWETE NA MAMA SALMA wahudhuria MAZISHI YA MZEE ZIMBIHILE - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

RAIS KIKWETE NA MAMA SALMA wahudhuria MAZISHI YA MZEE ZIMBIHILE

 
Raisi Jakaya Kikwete Na Mkewe Mama Salma Wakipita Mbele ya Jeneza Wakitoa Heshima Za Mwisho
Rais Dr. Jakaya Mrisho Kikwete akiweka udongo katika kaburi la kada wa CCM na mpigania uhuru, mzee David Zimbihile wakati wa mazishi ya kada huyo mkongwe (80) yaliyofanyika Muleba, Mkoani Kagera jana. Pichani juu:Mwenyekiti wa CCM, Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakitoa heshima za mwisho kwa marehemu mzee David Zimbihile wakati wa ibada ya mazishi iliyofanyika Muleba jana jioni. Mzee Zimbihile aliyewahi kuwa mbunge na kushika nyadhifa mbalimbali katika Chama Cha Mapinduzi alizikwa kwa heshima zote kijijini mwake Muleba, mkoani Kagera.
Mwenyekiti wa CCM, Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakiweka shada la maua katika kaburi la mpigania uhuru na kada mkongwe wa CCM, David Zimbihile wakati wa mazishi yake yaliyofanyika Muleba, mkoani Kagera jana jioni. Marehemu Zimbihile alianza harakati za ukombozi wa mwafrika nchini Kongo (DRC) ambapo alifanya kazi kwa karibu na Marehemu Patrice Lumumba na baadaye kupitia vyama vya wafanyakazi alikutana na Marehemu Kwame Nkurumah na hatimaye alirejea nchini Tanzania kuendelea na harakati hizo.
Picha na Freddy Maro

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages