GRAND Malt Yaimwagia timu ya Baraza la Wawakilishi Vifaa Vya Michezo Vyenye Thamani Ya Shilingi Mil 10 - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

GRAND Malt Yaimwagia timu ya Baraza la Wawakilishi Vifaa Vya Michezo Vyenye Thamani Ya Shilingi Mil 10


 Waziri wa Habari, Utalii,Utamaduni na Michezo, Abdilah Jihad (kushoto)akipokea jezi kutoka kwa Meneja wa kinywaji  kisicho na kilevi cha GrandMalt, Consolata Adam kwa ajili ya timu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibaritakayopambana na timu ya Klabu ya  Wazee ya Arusha Septemba 8,mwaka huu. Anayeshuhudia katikati ni Makamu Mwenyekiti wa timu ya Baraza, Mbarouk Mussa. Grand Malt ambayo imetoa vifaa hivyo vya michezo vyenye thamani ya sh. milioni 10, ni wadhamini wa  bonanza italoshirikisha pia vilabu vingine vya veterani.
Meneja wa kinywaji kisicho na kilevi cha Grand Malt, Consolata Adam(kulia)akihutubia katika  hafla hiyo.
Waziri wa Habari,Utalii, Utamaduni na Michezo,Abdilah Jihad  akitangaza rasmi kuwa kinywaji kisicho na kilevi cha Grand Malt kimeruhusiwa kudhamini michezo na shughuli mbalimbali kisiwani Zanzibar. Alitangaza
jana mjini Zanzibar wakati  Grand Malt ilipotoa vifaa vya michezo vyenye thamani ya sh. milioni 10 kwa ajili ya bonanza la veterani litakalofanyika Arusha Septemba 8, mwaka huu. Kulia ni Meneja wa kinywaji hicho,
Consolata Adam na Makamu Mwenyekiti wa timu ya baraza, Mbarouk Mussa.
Waziri wa Habari,Utalii, Utamaduni na Michezo, ambaye pia ni Mwenyekiti wa timu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Abdilah Jihad akiwa na baadhi ya viatu walivyokabidhiwa.
Waziri wa Habari,Utalii, Utamaduni na Michezo, ambaye pia ni Mwenyekiti wa timu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Abdilah Jihad (wa pili kushoto), Makamu Mwenyekiti wa timu hiyo, Mbarouk Mussa
(kushoto), pamoja na Meneja wa kinywaji kisicho na kilevi cha Grand Malt, Consolata Adam (kulia) wakigongeana kopo za kinywaji hicho wakati wa hafla ya timu hiyo kukabidhiwa vifaa vya michezo vyenye thamani ya sh. milioni 10, mjini Zanzibar jana.
wageni waalikwa wakiwa katika hafla hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Baraza la wawakilishi.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages