Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akiwa katika mahojiano na mtangazaji wa Redio ya Umoja wa Mataifa (UN),
Flora Nducha, muda mfupi baada ya kuhudhuria mkutano wa majadiliano
kuhusu masuala ya ukimwi ulioandaliwa na Umoja wa Mataifa unaofanyika
jijini New York.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib
Bilala, akisalimiana na mtangazaji wa Redio ya Umoja wa Mataifa (UN)
Flora Nducha, wakati mtangazaji huyo alipofika kwa ajili ya kufanya
mahojiano naye kuhusu maudhui ya mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu Ukimwi uliofanyika jijini New York.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akiwa na baadhi ya viongozi wenzake kutoka nchi mbalimbali wakati
akishiriki mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu Ukimwi unaofanyikajijini
New York.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akiwa katika picha ya pamoja na mshauri Mkuu wa ufundi na Asasi ya
Viongozi wa Afrika inayohusika na vita dhidi ya Malaria, Dkt. Melanie
Renshaw (wa pili kulia) na Balozi wa Tanzania wa Umoja wa Mataifa,
Ombeni Sefue (kulia) na Mkurugenzi wa Sekretarieti ya Umoja wa Mataifa
inayohusika na vita dhidi ya Malaria, Saleemah Abdul-Ghafur (kushoto),
wakati walipomtembelea Makamu wa rais jijini New York Juni 9 na kufanya
mazungumzo.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Tacaids, Dkt. Fatma
Mrisho (kushoto) na Mkurugenzi wa Tume ya Ukimwi Zanzibar, Dkt. Omari
Shauri (kulia) wakati walipomtembelea Makamu wa rais jijini New York, na
kufanya mazungumzo.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)