Baada ya kuitambulisha vyema Usiku wa Kopo kwa wakazi wa Dodoma na
viunga vyake, Kampuni ya Entertainment Masters Limited magwiji wa
burudani nchini, wameamua kuongeza burudani kwa kumshusha rais wa
wasafi Diamond Platinum kwenye shoo maalum kwa ajili ya wakaazi wa Dodoma.
Usiku huu maalum ujulikanao kama usiku wa Kopo
itatawaliwa na nderemo, muziki na vinywaji mbali mbali vya kopo. Lengo
haswa ni kuwapa wakaazi wa Dodoma burudani. Usiku wa Kopo na Diamond itafanyika tarehe 4 Juni 2011 katika Ukumbi wa Royal Village.
Mbali
na burudani toka kwa Diamond Platinum, pia kutakuwepo na burudani
mbalimbali ili kukidhi kiu ya burudani ya wakaazi wa Dodoma.
Pia kwa kutambua ya kwamba wanafunzi wa vyuo mbali mbali wanahitaji burudani, EML itatoa usafiri wa kwenda na kurudi kwenye kila chuo.
Usiku wa Kopo itawakutanisha wanafunzi wa vyuo na kuwapa fursa ya kubadilishana mawazo.
Pia kwa kutambua ya kwamba wanafunzi wa vyuo mbali mbali wanahitaji burudani, EML itatoa usafiri wa kwenda na kurudi kwenye kila chuo.
Usiku wa Kopo itawakutanisha wanafunzi wa vyuo na kuwapa fursa ya kubadilishana mawazo.
Muziki
katika Usiku wa Kopo itaporomoshwa na MaDJ toka Club Maisha ya jijini
Dar es Salaam. Madj hao mahiri ni DJ Zero, DJ S-Dizo na Hyperman HK. Mbali na burudani mbalimbali pia kutakuwepo na zawadi kutoka kwa
Wadhamini.
Penniel Mungilwa
Meneja Uhusiano





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)