WASIFU WA OSAMA BIN LADEN - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

WASIFU WA OSAMA BIN LADEN


Mwanzilishi na kiongozi wa kundi la kigaidi la Al-Qaeda, Osama Bin Laden, ameuwawa na majeshi ya Marekani nchini Pakistan, rais Obama amesema.

kwa mujibu wa taarifa za kijasusi, zinasema kuwa kiongozi huyo wa al-qaeda aliuwawa katika operesheni ya ardhini nje ya mji wa Islamabad.
Akitoa taarifa ya kuuawa Rais wa Marekani, Obama amesema baada ya ufyatulianaji wa risasi, majeshi ya Marekani ilichukua mwili wake.

 WASIFU WA OSAM BIN LADEN

Osama bin Laden alizawa mwaka wa 1957, katika familia ya kitajiri nchini Saudi Arabia. Ana zaidi ya mandugu na dada 50. Babake Osama alimiliki kampuni kubwa ya ujenzi. Katika baadhi ya picha zake za utotoni, Osama ameonyeshwa akiwa na mavazi ya kifahari na ghali, akiwa likizoni katika miji mbali mbali barani Uropa.
Hata hivyo mwanzoni mwa miaka ya themaninialiyupia mgongo maisha haya ya starehe na kitajiri, ana kujiunga na vugu vugu la kupigania haki dhidi ya utawala wa kisovieti baada ya majeshi yake kuishambulia Afghanistan.
Na hapo akipigana pamoja na waarabu wenzake, ndipo alizindua kundi la kigaidi la Al qaeda. Mnamo mwaka wa 1998, alitangaza fatwa yaani vita vikali vya kidini dhidi ya Marekani. Kufuatia ghadhabu aliyokuwa nayo na Marekani, kwa kuweka majeshi yake katika ardhi ya kiislamu, katika nchi mbali mbali mashariki ya kati.
Alioa mke wake wa kwanza akiwa na miaka 17, na baadaye akawaoa ya wake wengine wanne. Osama Bin Laden naaminiwa kuwa na watoto 17.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages