(THE CONSTITUTIONAL REVIEW BILL, 2011)
Kwa mujibu wa Kanuni ya 114(9) ya kanuni za kudumu za Bunge, kamati ya Bunge ya Katiba, sheria na Utawala Bora inawaalika wananchi na wadau wote kushiriki katika mkutano wa kupokea maoni kuhusu Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya katiba ili kupata maoni na ushauri wao kwa ajili ya kuboresha Muswada huo.
Mikutano ya kupokea maoni hayo itafanyika tarehe 7, 8 na ikibidi tarehe 9 April, 2011 Mjini Dar es salaam na Dodoma kama jedwali hapa chini linavyoonyesha:
S/N SIKU MKOA UKUMBI MUDA
7 – 8/April/2011 Dar es salaam Karimjee Saa 3 Asubuhi
7 – 8/April/2011 Dodoma Msekwa
Kwa taarifa hii, wananchi wote kwa ujumla wanaalikwa kushiriki kwenye mikutano hii kwa ajili ya kutoa maoni yao kama inavyoonekana katika jedwali hapo juu.
Imetolewa na:
Ofisi ya Bunge
Idara ya Habari, Elimu kwa Umma na Uhusiano wa Kimataifa
Dar es Salaam
5 Aprili 2011





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)