Waziri wa Afya, Dk.Haji Mponda (pichani) ameahidi kupiga mzigo na mastaa 10 wa muziki wa Kizazi Kipya nchini, wanatambulika kama Mabalozi wa ‘Malaria No More’.
Akizungumza na Ijumaa ofisini kwake, Posta jijini Dar es Salaam hivi karibuni, Mheshimiwa Mponda aliwataka mabalozi hao kutunga nyimbo za hamasa na kubadili tabia ya kuudharau Ugonjwa wa Malaria iliyojengeka miongoni mwa watu.
Mponda aliwataka wasanii hao kutafuta njia mpya za kusambaza ujumbe kuhusu kujikinga na ugonjwa huo.
“Niko tayari kushirikiana nao, lakini nawaomba kutunga nyimbo zenye hamasa na pia kutafuta njia mbadala za kuhamasisha watu waelewe zaidi kuhusu ugonjwa huu, wakati mwingine unaweza kuona mtoto ana dalili zote za Malaria lakini mama yake anampa dawa za kutuliza maumivu kisha anaendelea na shughuli zake, hii ni kwa sababu ya uelewa mdogo,” alisema Mponda.
Wasanii waliopo katika programu hiyo ni Judith Wambura ‘Lady Jaydee’, Joseph Haule ‘Profesa Jay’, Mwasiti Almas, Amini Mwinyimkuu na Banana zorro.
Wengine ni Naseeb Abdul ‘Diamond’ Lawrence Marima, Barnaba Elias, Fareed Kubanda ‘Fid Q’ na Sunday Mangu ‘Linex’.





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)