KONGAMANO LA MAWAKALA WA NMB LAFANYIKA DAR, WAPEWA ELIMU ZA KIBENKI - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

KONGAMANO LA MAWAKALA WA NMB LAFANYIKA DAR, WAPEWA ELIMU ZA KIBENKI

DSC_1401
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam na Zanzibar, Badru Idd akizungumza na mawakala wa Benki ya NMB walioshiriki kwenye kongamano la mawakala wake wanaotoa huduma za kifedha maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam.

DSC_0073
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam na Zanzibar, Badru Idd (kulia) akimkabidhi mmoja wa mawakala wa Benki ya NMB cheti kwenye semina ya mawakala wake wanaotoa huduma za kifedha maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam.

DSC_0055
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam na Zanzibar, Badru Idd (kulia) akimkabidhi mmoja wa mawakala wa Benki ya NMB cheti kwenye semina ya mawakala wake wanaotoa huduma za kifedha maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam.

DSC_0051
Ofisa Mkuu wa Kitengo cha Mawakala wa Benki ya NMB, Ericky Willy (wa pili kulia) akimpongeza kabla ya kukabidhiwa cheti mmoja wa mawaka aliyehudhuria semina ya mawakala wa Benki ya NMB wanaotoa huduma za kifedha maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam.


DSC_0287
Sehemu ya mawakala wa NMB waliohudhuria kongamano hilo wakionesha vyeti vyao mara baada ya kukabidhiwa.

DSC_0028
Mawaakalaa wakiwa katika kongamano hilo.

DSC_0004
Mada mbalimbali zikiwasilishwa na maofisa wa Benkli ya NMB

DSC_1444
Ofisa Mkuu wa Kitengo cha Mawakala wa Benki ya NMB, Ericky Willy akizungumza kwenye semina ya mawakala wa Benki ya NMB wanaotoa huduma za kifedha maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam.

DSC_0294
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam na Zanzibar, Badru Idd na Meza kuu kwenye semina kwa mawakala wa Benki ya NMB wa jijini Dar es Salaam wakipiga picha ya pamoja na mawakala bora kwa mwaka 2018 wa Benki hiyo kwa kanda ya Dar es Salaam.


BENKI ya NMB leo imefanya kongamano la mafunzo kwa mawakala mbalimbali wanaotoa huduma za kibenki kwa wateja wa benki hiyo, lengo likiwa ni kuboresha huduma zake na kuwajengea uwezo wa kibiashara mawakala hao.

Akizungumza katika kongamano hilo lililofanyika Sinza jijini Dar es Salaam, Meneja wa Kanda ya Dar es Salaam na Zanzibar, Badru Idd alisema benki hiyo itaendelea kuwajengea uwezo mawakala hao kwani wao ni sehemu ya benki hivyo huduma zao zinatakiwa kufafana na zinazotolewa kwenye matawi yao.

Aliwataka kuendeleaa kutoa huduma kwa uaminifu kwa wateja na kuzingatia taraatibu walizopewa na Benki ili wateja wanaowahudumia waendelee kuiamini benki yao. Aliongeza NMB itaendelea kuboresha huduma zake na kuendelea kuwa kinara katika sekta ya fedha nchini.

Katika kongamano hilo la kuwajengea uwezo mawakala wa NMB ikiwa ni muendelezo wa semina hizo nchi nzima, NMB imetoa zawadi na vyeti kwa mawakala wanaofanya vizuri katika kutoa huduma kwa wateja ili kuwapa motisha ya kuendelea kufanya vizuri.

Akitoa mafunzo kwa mawakala, Meneja Mwandamizi wa NMB Wakala, Tito Mangesho alisema mikakati ya NMB ni kuongeza idadi ya wateja huku ikitumia njia rahisi na salama ya kuwahudumia kiufanisi zaidi.

Aidha aliongeza kuwa malengo mengine ni pamoja na kuongeza unafuu wa gharama zake na uharaka wa kuwahudumia wateja, kupunguza msongamano na kuboresha kamisheni kwa mawakala wake.

Naye, Meneja wa NMB Wakala Kanda ya Dar es Salaam, Kisamo Edwin aliongeza kuwa miongoni mwa matarajio ya NMB hapo baadaye ni kuleta mashine mpya za kisasa kwa mawakala zitakazo kuwa na wigo mpana wa kutoa huduma na kumuongezea kipato.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages