SIKU SABA ALIZOTOA WAZIRI KIGWANGALLA ZAZAA MATUNDA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

SIKU SABA ALIZOTOA WAZIRI KIGWANGALLA ZAZAA MATUNDA

Wiki chache zilizopita Waziri wa Maliasili na Utalii Dk Hamisi Kigwangalla alitoa siku saba kwa polisi kukamata watuhumiwa wa mauaji ya mwanaharakati dhidi ya mauaji tembo Wayne Lotter, pia alitaka nyumba zilizouzwa kinyemela huko Arusha zirudishwe na pia alitoa siku saba kwa wakurugenzi wa kampuni nne za uwindaji kukutana nae Dodoma.

Jana kwenye kipindi cha 360 Waziri Dk. Kigwangalla alitoa maelezo ya kina kuhusu maelekezo aliyotoa na pia kuelezea mikakati mbalimbali ya Wizara yake. Kuhusu mauaji ya Lotter alisema kuwa watuhumiwa walikamatwa na kufikishwa mahakamani. Alimsifu IGP Sirro kwa ushirikiano na Wizara yake.

Alieleza kuwa Katiba inatambua Waziri kama sehemu ya Serikali na kwamba Polisi wapo ili kusaidia Serikali kutimiza malengo yake. Kuhusu nyumba za Arusha, alieleza kuwa ushahidi unaonyesha wazi kuwa waliotajwa walikuwa wamiliki wao binafsi au kupitia familia zao. Waziri Dk.Kigwangalla alieleza mkakati wa kufungua na kukuza utalii kusini mwa Tanzania.

Alieleza mradi wa regrow ambao utawezesha sekta ya kukua kusini mwa Tanzania. Pia alizung umzia umuhimu wa uhifadhi na kueleza kuwa mto Ruaha kwa sasa unakauka kwa siku 60 wakati wa kiangazi na malengo ni kurejesha hadi kukauka kwa siku 10 tu. Kuhusu kutangaza vivutio, Waziri Dk.Kigwangalla alieleza mkakati wa kutangaza vivutio na pia uanzishwaji wa mwezi wa urithi ambao sio tu utaongeza vivutio vya utalii bali utaenzi tamaduni na mila za Kitanzania.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages