SOMO LA KWANZA LA DIGITALI LEO JUMATATU: MAWASILIANO YA SATELITE - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

SOMO LA KWANZA LA DIGITALI LEO JUMATATU: MAWASILIANO YA SATELITE

Picha ya Satelite aina ya SPUTNIK 1 
MAWASILIANO YA SATELAITI 

Satelaiti ni nini?  
Nikifaa (mashine au mtambo) ambao huwekwa angani kuzunguka dunia au kitu chochote kilichoko angani.
 
Satelaiti ya kwanza kutengenezwa na binadamu, kupelekwa angani na kuwekwa katika obiti kuzunguka dunia iliitwa 
 
 SPUTNIK 1.
Ilitengenezwa na Urusi na kupelekwa angani tarehe 4 Octoba, 1957. Satelaiti hii ilisafiri kwa mwendo wa kilomita 29,000(km) kwa saa ikitumia dakika 96.2 kukamilisha mzunguko wa dunia. Ikiwa angani ilituma mawimbi ya mawasiliano katika masafa ya 20.002MHz na 40.002MHz ambayo yalipokelewa na mitambo ya redio za amateur “amateur radio” duniani kote. Iliendelea kutuma mawimbi kwa siku 22 baadaye nguvu ya betri za transmita hizo ziliisha nguvu tarehe 26 Octoba, 1957. Satelaiti hiyo ilianza kudondoka toka katika obiti angani na kuungua tarehe 4 Januari, 1958 baada ya kuingia kwenye anga ya dunia (atmosphere). Ilikaa katika obiti kwa muda wa miezi mitatu.

Kuna satelaiti za aina ngapi?
 
Kuna satelaiti za aina mbili: 
1.      Satelaiti za asili (Natural satellites) mfano; Dunia (Dunia huzunguka Jua) na Mwezi (mwezi huzunguka Dunia).
 
2.      Satelaiti za kutengenezwa na Binadamu (Artificial satellites).

Kuna aina ngapi za Satelaiti za kutengenezwa na binadamu?

Zipo satelaiti za aina nyingi na zimetengwa kwa matumizi mbalimbali.

1.      Satelaiti kwa ajili ya utafiti na uchunguzi sayari za mbali, galaxies na vitu vingine vinavyoelea angani (Astronomical satellites).
 
2.      Satelaiti zinazowekwa angani kwa ajili ya kufanya mawasiliano (Communications Satellites).
 
3.      Satelaiti zinazowekwa angani kwa ajili ya kuangalia hali ya hewa (Weather Satellites).
4.      Satelaiti zinazowekwa angani kwa ajili ya matumizi ya Ki-intelijensia na Kijeshi (Intelligence and Military Operations Satellites).
 
5.      Satelaiti zinazowekwa angani kwa ajili ya kufanya utafiti wa dunia na vitu vingine vilivyoko angani mfano (Biosatellites ambazo hubeba viumbe hai kwenda angani kwa ajili ya utafiti).
 
6.      Satelaiti zinazowekwa angani kwa ajili ya kufuatilia mabadiliko ya dunia na mazingira (Earth Observational Satellites).
 
7.      Ofisi za uchunguzi wa anga zinazoelea angani (Space Stations).
 
8.      Vifaa (mitambo) vyote vinavyokuwa angani katika obiti (Manned Spacecrafts / Spaceships).
 
9.      Satelaiti ndogo zinazounganishwa katika satelaiti nyingine kwa waya mwembamba unaoitwa tether (Tether Satellites)
 
10.  Satelaiti kwa ajili ya kutambua (mahali/ sehemu) katika uso wa dunia (positioning satellites) mfano GLONASS ni mfumo wa Urusi, GPS (Global Positioning System) ni mfumo wa Marekani, GALILEO ni mfumo wa Ulaya (European Union), China mfumo wao COMPASS (Compass Navigation System).

Satelaiti tunazozitumia kupokea mawimbi ya televisheni / redio zipo katika kundi la Satelaiti za Mawasiliano (Communication Satellites).

Satelaiti hizi za mawasiliano tunazozitumia kupitisha mawasiliano ya televisheni na redio (zipo katika Geosynchronous Orbit) umbali wa kilomita 35,786km kutoka ardhini katika Ikweta na husafiri kwa kasi sawa na kasi ya dunia.

MAWASILIANO KUTOKA SATELAITI ZA MAWASILIANO ZILIZOPO KATIKA "GEOSYNCHRONOUS ORBIT"

KUTAFUTA CHANELI MBALIMBALI ZA TELEVISHENI / REDIO KUTOKA KATIKA SATELAITI MBALIMBALI ZA MAWASILIANO ZILIZOPO KATIKA GEOSYNCHRONOUS ORBIT ; OBITI AMBAYO KWA MAJINA MENGINE HUITWA (PARKING ORBIT au CLARKE BELT au GEOSYNCHRONOUS ARCH)

Kwa kuwa dunia ina umbo la duara si rahisi watu wote tulioopo katika uso wa dunia (namaanisha mabara yote) tukatumia satelaiti moja kupokea mawasiliano toka katika satelaiti. Kusema hivi namaanisha mfano satelaiti tunayoitumia sana (IS 906 @ 64.2E (nyuzi za longitudo 64.2 Mashariki mwa Greenwich) katika ukanda wetu Tanzania ikiwemo haiwezi kufikisha mawimbi yake Marekani kwa sababu Marekani wanakuwa upande mwingine wa uso wa dunia (they are below the horizon of the reach of that satellite) hii ni vile vile kwa satelaiti zinazoimulika Marekana hata sisi hatuwezi kupata mawimbi yake. Mfano baadhi ya satelaiti za Intelsat (IS 902, IS 906, IS 904, IS 10, IS 17, IS 907 na nyinginezo zilizoko juu ya usawa wa Afrika na bahari ya Hindi na wao wakitaka kupokea mawasiliano yake wanatumia kituo chao (kilichopo Afrika Kusini).

Baadhi ya satelaiti ambazo mawimbi yake yanafika hapa Tanzania zipo kati ya nyuzi za longitudo 27 Magharibi mwa Mstari wa Greenwich na nyuzi za longitudo 85 Mashariki mwa Mstari wa Greenwich. Dishi linalozunguka (horizon to horizon) linaweza kupata chaneli mbalimbali kutoka satelaiti hizi kwa kuzunguka kupitia satelaiti moja baada ya nyingine (from 27 West to 85 East). Kadri unavyoelekea Magharibi ndivyo utakavyozidi kupata satelaiti zilizopo Magharibi huku ukipoteza za Mashariki; na kinyume chake (and vice versa).

Baadhi ya satelaiti ambazo zinazunguka kwa kasi sawa na kasi ya dunia; ambazo zipo katika "Geosynchronous Orbit or Parking Orbit" zinazopatikana katika eneo letu (Tanzania na nchi za jirani zimeorodheshwa chini. Satelaiti hizi hutumika kwa mawasiliano mbalimbali mfano Data /Internet, Televisheni, Radio, Mawasiliano ya Ki-intelijensia, kijeshi na mawasiliano mengine.

Intelsat 907 @ 27.5W:
VoA TV, Alhurra TV Iraq, Alhurra TV Europe, RTG (Guinea),

Intelsat 905 @ 24.5W:
Nile Drama, Syria 1,

SES 4 @ 22W:
Bolivia Mux,

NSS7 @ 20W: 
CNN, TBN, Emmanuel TV),

Intelsat 901 @ 18W
: Ethiopia Educational Media Agency

Telstar 12 @ 15W:


Nilesat 102 @ 7W:
DW Arabia, BBC Arabic, Abu Dhabi, Abu Dhabi Sport 1, Dubai Sport 2, DM    TV, National Geographic Channel,

Intelsat 10 - 10W @ 1W:
 BBC World Service, RTS1 (Senegal)

Rascom QAF 1R @ 2.8E: 
Libya Satellite TV, Libyan Mux, RTNC, Digital Congo (Congo)

Eutelsat 7A @ 7E: Record Mozambique, MBC 1, MBC 2, CRTV, RTS 1 (Senegal), BBC Persian,
ORTM, Raha Tv, TPA Internacional, VoA TV Persian.

Eutelsat 10A @ 10E: 
Startimes, Agape TV Network,

Amos 5 @ 17E:
 Zambia Mux, Reuters Live, Doordarshan, Kingdom Africa TV, Bible Exploration TV, Fashion TV Europe,

Eutelsat 36A @ 36E:
TING Channels (Tanzania), NTV Plus, Afrique TV,

Eutelsat 36B @ 36E:
CCTV News, CCTV 4 Europe, Multichoice DStv channels

NSS 12 @ 57E:        
ZUKU, KBC- Kenya, Family TV - Kenya, ETV (Ethiopia), VoA TV Africa, Ameican Embassy tv Network etc.), 

Intelsat 904 @ 60E:
 Uganda Mux, Kenya Mux, NTV (Kenya), KBC Channel 1 (Kenya), TBC 1, NTV Uganda (Kenya), Swazi TV, ZNBC,

Intelsat 902 @ 62E:
NTV (Kenya), Citizen TV (Kenya), SABC 1 - 3 (South Africa), Sky News International,

Intelsat 906 @ 64.2E: ITV, EATV, CAPITAL, TBC, STARTV, TVM (Mozambique), UBC (Uganda), Chanel 10,

Intelsat 906 @ 64.2E inakofikisha Mawimbi yake katika masafa ya C Band (Hemi, Zonal & Global Beams)

Intelsat 17 @ 66E:
 HMTV, Captain TV, ABN (India), V6 News,

Intelsat 20 @ 68.5E:
Indiasign, NHK World TV (Japan), Peace TV Bangla, India TV, South Korea Mux, CTS (South Korea), Hope TV India, YTN World, VTV (India), Peace TV, God TV Africa, Africa Unite TV, ABN (Nigeria), Messiah TV, Citizen TV (Kenya), UB (South Africa), Emmanuel TV, CTV, 3ABN International, Press TV, CCTV, EWTN, 

Intelsat 7 @ 68.6:     Vivid, UNISA (South Africa), Botswana TV, SABC 1-3, ITV (S
outh Africa France 24 English, God TV Africa, Multichoice South Afica, 

Eutelsat 70A:            Canadian Forces Radio & TV, 
  ABS 1 @ 75E:

Apstar 7 @ 765E:      ERT World, Channel 9 (Bangladesh), God Asia, 


Thaicom 5 @ 785E:
   Somalia National TV, TV5 Cambodia, T Sports Channel, Shop Thailand, Spring.TV News, MRTV,  na nyinginezo. 

Express MD1 @ 80E:


Dishi linaloweza kufanya kazi hii vizuri ni la kipenyo kuanzia futi nane 8ft, 10ft, 12ft na kuendelea (hasa kuanzia futi kumi 10ft na kuendelea).

Kwa madishi ambayo hayazunguki (fixed satellite dishes) inabidi ufunge madishi mengi kila dishi liwasiliane na satelaiti yake. Ndio maana ukienda katika vituo vya televisheni/ redio mfano ITV, Startimes na vingine unakuta madishi mengi ya kupokea mawasiliano (chaneli) mbalimbail toka katika satelaiti tofauti tofauti.

Masafa ya Mawimbi ya Televisheni / Redio kwenda (uplink frequencies) katika satelaiti katika eneo letu ITU Region 1 (Afrika, Ulaya, Uarabuni na Urusi)
 
Masafa yanayotumika kupeleka mawimbi katika satelaiti toka vituo vya Televisheni/Redio vinavyotumia Ku Band katika ukanda wetu (ITU Region 1) ni kati ya 14.0GHz - 14.5GHz.

Masafa yanayotumika kupeleka mawimbi katika satelaiti toka vituo vya Televisheni/Redio vinavyotumia C Band katika ukanda wetu (ITU Region 1) ni kati ya 5.850GHz - 6.425GHz.
 
Tutaendelea Na Somo letu Jumatatu Ijayo usikose Kupitia Lukaza Blog 

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages