Wananchi wa shehia ya Kilombero iliyoko Wilaya ya Kaskazini B wameuomba Uongozi wa Jimbo lao, Wilaya na Serikali Kuu kuangalia uwezekano wa kuwapatia huduma ya Umeme - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wananchi wa shehia ya Kilombero iliyoko Wilaya ya Kaskazini B wameuomba Uongozi wa Jimbo lao, Wilaya na Serikali Kuu kuangalia uwezekano wa kuwapatia huduma ya Umeme

 
   Mwananchiwa Kijiji cha Kilombero Nd. Bakari Mtumwa Silima  akiwasilisha kilio cha Wananchi waKijiji  hicho cha ufinyu wa Huduma yaMaji safi mbele ya Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi hapo Skuli yaKilombero Wilaya ya Kaskazini B.
   NduguBakari Omar wa Shehia ya Kilombero akielezea kadhia inayowapata Watoto waokatika kivuko kinachojaa maji msimu wa masika wakati wanapokwenda kwenye masomoyao.
 Mbunge wa Jimbo la Kitope BaloziSeif Ali Iddi akijibu na kufafanua baadhi ya kero zinazowakabili wananchi waShehia ya Kilombero katika harakati zao za kila siku za maisha.Kulia ya Balozi ni Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini B Nd. Khamis Jabir Makame na Kushoto yake ni Mkewe Mama AshaSuleiman Iddi
Mbunge waJimbo la  Kitope Balozi Seif Ali Iddi akipeana mikono na Wananchi wa Shehia ya Kilombero mara baada ya kupokea kerona matatizo yanayowakabili Wananchi  hao
--
 
Wananchi wa shehia ya Kilombero iliyoko Wilaya ya Kaskazini B  wameuomba Uongozi wa Jimbo lao, Wilaya na Serikali Kuu kuangalia uwezekano wa kuwapatia huduma ya Umeme itakayosaidia kutanzua tatizo la maji linalowakabili kwa muda mrefu sasa.

Ombi hilowamelitoa mbele ya Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi aliyefika Kijijini hapo kusikiliza matatizo na kero zinazowakabili wananchi hao hapo katika  viwanja vya skuli ya Kilombero.

Ndugu Bakari Mtmwa Silima akiwasilisha Kero za Wananchi hao alimueleza Balozi Seif kwamba licha ya juhudi zinazochukuliwa naViongozi wa Jimbo hilo lakini bado  huduma ya Maji safi inaendelea kuwa mtihani kwao.

Nd. Bakari alisema harakati za uchimbwaji wa Kisima cha maji safi kwa ajili ya Wananchi wa Shehia hiyo unaendelea vyema lakini tatizo linalojitokeza ni upatikanaji wa huduma za umeme kufikia eneo hilo.

“ Utaratibu wa kupelekea umeme Kilombero juu  kilipo kisima hicho unafikia masafa ya Kilomita moja. Lakini mbali ya huduma hiyo ya maji pia sisi wananchi tunahitaji huduma hiyo kwa matumizi ya kawaida”. Alisisitiza Ndugu Bakari Mtumwa.

Naye Ndugu Bakari Omar alielezea kilio kinachowapata watoto wa eneo hilo cha ukosefu wa kivuko wakati wanapokwenda skuli hasa wakati wa msimu wa mvua kubwa.

Alisema kivuko kinacholigawa eneo la kitongoji chao naskuli ya Kilombero huzidiwa na maji wakati wa masika na kutishia maisha ya wanafunzi hao wakati wanapotaka kuvuka.

Akijibu hoja za Wananchi hao wa Shehia ya Kilombero , Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi aliwataka Wananchi hao kuendelea kuwa na ustahamilivu na juhudi zitaendelea kufanywa ili kuona huduma ya maji safi inapatikana kwa uhakika katika eneo hilo.

Alisema Uongozi wa Jimbo, Wilaya na Hata Serikali Kuu unaelewa tatizo la usumbufu wa huduma ya maji safi unaowapata Wananchi wa Kilombero.

 “ Ukweli usiofichika kwamba maji ni uhai wa kilakiumbe. Kwa kulifahamu hili mimi binafsi ninaposikia kiliocha maji katikamaeneo maeneo yoyote Nchini huamua kulivalia njuga hadi lifikie ufanisi”.Alisisitiza Balozi Seif.

Balozi Seif aliwahakikishia Wananchi hao kwamba yeyena viongozi wenzake wa Jimbo watafanya jitihada za kuwasiliana na Taasisi mbalimbali ili kuona namna gani wanaweza kusaidiana kulitatua tatizo la Umeme ambalokwa sasa linahitaji uwezo wa ziada.

“ Licha ya uchimbwaji wa Kisima hicho cha maji kuondoatatizo la Wananchi hao lakini bado kazi iliyopo hivi sasa ya huduma ya umemeinahitaji gharama kubwa”. Alisisitiza Balozi Seif.

Alisema upo uzoefu unaoonyesha kwamba tatizo laukosefu wa maji safi katika maeneo mengi linaonekana kusababishwa na nguvu ndogo zinazotokana na mashine  zinazowekwa kwenye visima vya maji.

Akizungumzia kivuko kiliopo kati ya  Kilombero Skuli na Kilombero Juu Balozi Seif aliagiza kupatiwa makisio ya gharama za kazi ya Matengenezo ya eneo hilo muda wowote kuanzia sasa ili kukamilisha kazi hiyo na kutoa faraja kwa watoto na wakaazi wa eneo hilo.

Balozi Seif alisema hatua ya kuondosha usumbufu huoinawezekana kukamilishwa ndani ya wiki moja baada ya  kupatikana kwa Kifusi na  Makalvati.

Mapema Mke wa Mbunge wa Jimbo Hilo la Kitope Mama Ash aSuleiman Iddi aliwakumbusha Wananchi hao kuendelea kuthamini juhudi zinazochukuliwa na Viongozi wao katika kuwatatulia kero zinazowakabili.

Uchimbaji wa kisima cha Maji safina salama kwa ajili ya Shehia hiyo ya kilombero unaendelea katika eneo la Kilombero juu ukigharamiwa na Mbunge wa Jimbo hilo.
 
Na
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages