Taswira Mbalimbali Kutoka Maonyesho ya Wakulima Nanenane Mkoani Dodoma - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Taswira Mbalimbali Kutoka Maonyesho ya Wakulima Nanenane Mkoani Dodoma

 Mtunzaji Kumbukumbu na Mhasibu Abbas Mnyeto wa Wizara ya Fedha wakiwasaidia wazee wastafu upande wa Kilimo juu ya taratibu za kupata pesheni kwa watumishi wanapostaafu jana mjini Dodoma walipokuwa kwenye banda la Wizara hiyo kwenye maonyesho ya wakulima nanenane.
  Afisa Malipo ya Pesheni wa Mfuko wa Pesheni kwa watumishi wa umma (PSPF) Andrew Dayson (kushoto) akiwasidia Maafisa Polisi kujua kiwango michango yao mbalimbali ambayo wamekwishachangia tangu waingie katika utumishi wa umma wakati walipotembelea banda la Wizara ya Fedha kwenye maonyesho ya wakulima ya nanenane jana mjini Dodoma.
 Kaimu Afisa Uhusiano wa wa Mfuko wa Pesheni kwa watumishi wa umma (PSPF) Hawa Kikeke(kushoto) na Afisa Malipo ya Pesheni wa Mfuko wa Pesheni kwa watumishi wa umma (PSPF) Andrew Dayson (wa pili kutoka kushoto) wakiwasaidia Maafisa wa Polisi juu ya kupata taarifa za michango yao mbalimbali ambayo wamekwishachangia tangu waingie katika utumishi wa umma wakati walipotembelea banda la Wizara ya Fedha kwenye maonyesho ya wakulima ya nanenane jana mjini Dodoma.
 Afisa Uhusiano wa Chuo Mipango Dodoma Sarah Mmari (kushoto) akimwelimisha Yulis Otto (kulia) utaratibu wa kujiunga na masomo katika Chuo hicho wakati mzee huyo alioptembelea banda la Wizara ya Fedha jana katika maonyesho yanayoendelea mjini Dodoma.
 Afisa Uhusiano wa Chuo Mipango Dodoma Sarah Mmari (kushoto) akimwelimisha Yulis Otto (kulia) utaratibu wa kujiunga na masomo katika Chuo hicho wakati mzee huyo alioptembelea banda la Wizara ya Fedha jana katika maonyesho yanayoendelea mjini Dodoma.
 Afisa Masoko kutoka Dhamana ya Uwekezaji Tanzania (UTT) Said Mkomwa(kulia) akiwaelimisha wananchi faida za kuwekeza katika mifuko iliyoanzishwa na Dhamana ya Uwekezaji Tanzania jana mjini Dodoma walipotembelea banda la Wizara hiyo kwenye maonyesho ya wakulima nanenane.
 Mwanasheria kutoka Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana Emilia Mkubulo(kulia) akimwelimisha mmoja wa wananchi faida za kununua hisa jana mjini Dodoma alipotembelea banda la Wizara hiyo kwenye maonyesho ya wakulima nanenane.
 Afisa Uendeshaji wa Mfuko wa Pesheni kwa watumishi wa umma (PSPF) Kahenga Maulid( wa pili kutoka kulia) na Afisa Malipo ya Pesheni wa Mfuko wa Pesheni kwa watumishi wa umma (PSPF) Andrew Dayson (wa pili kutoka kushoto) wakiwasaidia watumishi wa Chuo kikuu cha Dodoma (UDOM) Monica Kung’aro (kushoto) na Mary Kulwijila(kulia) juu ya kupata taarifa za michango yao mbalimbali ambayo wamekwishachangia tangu waingie katika utumishi wa umma wakati walipotembelea banda la Wizara ya Fedha kwenye maonyesho ya wakulima ya nanenane jana mjini Dodoma.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages