Kamati ya Taasisi 4 za kiraia yaipa serikali siku 7 kuruhusu gazeti la MwanaHalisi Kuchapishwa - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Kamati ya Taasisi 4 za kiraia yaipa serikali siku 7 kuruhusu gazeti la MwanaHalisi Kuchapishwa

Mwnyekiti wa MISA-Tanzania Mohamed Tibanyendera, akizungumza na waandsihi wa habari kuhusu hatua wanazozichukua dhidi ya Serikali kutokana na kulifungia gazeti la MwanaHalisi.
---
Kamati ndogo iliyoundwa na taasisi nne za kiraia nchini ambayo inaratibu kupigania haki ya kufunguliwa kwa gazeti la MwanaHalisi, leo imeipa serikali siku saba kuliruhusu gazeti hilo kuendelea kuchapishwa.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa kamati hiyo Marcossy Albanie, amesema hawana sababu yakwenda mahakamani juu ya jambo hilo kwasababu hata serikali haikutumia njia hiyo ya mahakamani kwani ilikuwepo badala yake wametumia sheria kandamizi ya vyombo vya habari inayopigiwa kelele na wadau wa habari.

Kamati hiyo inayoungwa mkono na taasisi tano za kiraia baadhi ya taasisi hizo ni MISA TANZANIA, TANZANIA HUMANRIGHTS DEFENDERS COALITIONS NA KITUO CHA SHERIA NA HAKI ZA BINADAMU (LHRC) imeitaka serikalikutekeleza madai yafuatayo:-
  1. Kuitaka serikali kulifungulia gazeti la Mwanahalisi maramoja.
  2. Serikali badala ya kushughulikia Watetezi wa haki na wanahabari wanaofichua uovu ishughulike na wahalifu waluiomteka Dkt. Ulimboka.
  3. Serikali iache kabisa na ukandamizaji huu wa haki na uhuru wa habari.

WAANDISHI WA HABARI WAOMBWA YAFUATAYO SERIKALI ISIPOTEKELEZA HAYO:
  1. Kutochapisha habari yoyote itakayo wahusu Waziri wa Habari wa Wizara hiyo na Naibu wake, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo.
  2. Kusimama kidete kuunga mkono harakati hizo hadi zinapata ufumbuzi wake.
Ikumbukwe kesi Na.34/2009 iliyofunguliwa tangu 2008 kupinga sheria ya magazeti ya 1976 iliyotumika kufungia MwanaHalisi haijasikilizwa mpaka sasa.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages