Mabingwa
wa Soka Tanzania bara na Urafiki, Simba ya Dar es Salaam hadi sasa ipo
nyuma kwa goli moja dhidi ya URA ya Uganda katika mchezo wa Makundi
Kombe la Kagame.
Mashabiki wa timu ya Simba wakiwa wamefurika katika uwanja wa Taifa kujionea timu yao ikicheza na Waganda URA FC.
Derrick Walulya mchezaji wa timu ya URA FC kutoka nchini Uganda ambaye
aliwahi kuchezea timu ya Simba pia ya Tanzania akimiliki mpira mbele ya
Felix Sunzu mshabuliaji wa timu ya Simba katika mchezo wa kuwania kombe
la Kagame linaloandaliwa na Shirikisho la Vyama vya michezo Afrika
Mashariki CECAFA unaochezwa kwenye uwanja wa Taifa jioni hii mpaka sasa
mpira umekwisha na timu ya URA imeifunga timu ya Simba magoli 2-0.
magoli hayo yamefungwa na mchezaji Feni Ali wa URA FC.Picha Kwa Hisani ya Father Kidevu na Full Shangwe Blog
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)