Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo amekutana na kufanya mazungumzo na
Askofu Mkuu Protase Rugambwa ambaye hivi karibuni aliteuliwa na Baba
Mtakatifu Benedict wa XVI kuwa Katibu Mwambata wa Idara au Kongregasio
ya Uenezaji wa Injili kwaajili ya Mataifa na Rais wa Mashirika ya
Kipapa ya Kimisionari yenye makao yake, Roma.
Wakati
wa mazungumzo hayo Rais Kikwete kwa mara nyingine tena,amempongeza
Askofu Rugambwa kwa uteuzi wake na kusema kuwa uteuzi huo ni kielelezo
dhahiri cha imani kubwa aliyonayo Baba Mtakatifu kwa askofu huyo na
kuwa ni heshima kubwa kwa mtanzania kupata nafasi ya kushika wadhifa
huo mkubwa.Kabla ya Uteuzi huo Askofu mkuu Rugambwa alikuwa askofu wa
jimbo Katoliki Kigoma.Picha na Freddy Maro.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)