RAIS KIKWETE ATEMBELEA SHAMBA LA MFANO KIJIJI CHA CHIKOPELO BAHI, MKOANI DODOMA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

RAIS KIKWETE ATEMBELEA SHAMBA LA MFANO KIJIJI CHA CHIKOPELO BAHI, MKOANI DODOMA

 Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akikagua  shamba la nyanya  na mazao mengine ya mboga pamoja na mizabibu katika shamba linalomilikiwa na kampuni ya kilimo ya Tendaji Trade, lililopo kijiji cha Chikopelo,wilaya ya Bahi, Mkoani Dodoma  leo asubuhi. Kushoto ni mmoja wa wamiliki wa Shamba hilo Bwana Alon Hoven, anayeshirikiana na Bwana Dunstan Mrutu (hayupo pichani). Shamba hilo linamwagiliwa kwa kutumia teknolojia ya  matone (Drip irrigation system).
 Mmoja wa Wamiliki wa Shamba la Mboga katika kijiji cha Chikopelo Bwana Alon Hoven, kimwonesha Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, baadhi ya mazao yanayozalishwa kwa kutumia mbegu bora pamoja na teknolojia ya ya umwagiliaji wa matone wakati Rais alipotembelea shamba hilo katika kijiji cha Chikopelo, wilayani Bahi,mkoani  Dodoma leo asubuhi.Shamba hilo lenye ukubwa wa hekari mia moja linamilikiwa na kampuni ya kilimo ya Tendaji Trade, chini ya Bwana Dunstan Mrutu na Alon Hoven raia wa Israel.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Rais Kikwete alisifu juhudi za wawekezaji hao kwa kutumia mbinu za kisasa za kilimo na kuwaasa wanakijiji wa Chikopelo kujifunza mbinu bora za kilimo hicho cha mboga ili waweze kupata ufanisi na kuboresha maisha yao. Rais Kikwete alitumia fursa hiyo kuwaonya viongozi wa kijiji cha Chikopelo kutoendelea kuuza ardhi yote kwa wawekezaji na badala yake kutunza na kuilinda kwaajili ya kizazi kijacho.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages