RAIS KIKWETE ACHANGISHA BILIONI 3.2 KATIKA HARAMBEE YA KUCHANGIA MKAPA HIV/AIDS FOUNDATION - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

RAIS KIKWETE ACHANGISHA BILIONI 3.2 KATIKA HARAMBEE YA KUCHANGIA MKAPA HIV/AIDS FOUNDATION

ais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Bw. Deo Mwanyika, Makamu wa Rais wa Kampuni ya Barrick Tanzania baada ya kuibuka mchangiaji mkubwa kwa kutoa dola za Kimarekani laki 5 kwa ajili ya kuchangia taasisi ya Mkapa Hiv/Aids Foundation Jumanne Juni 5, 2012 usiku katika hoteli ya Kilimanjaro jijini Dar es salaam. Kushoto ni Rais Mstaafu  wa Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi na kulia ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mzee Benjamin William Mkapa aliyeandaa hafla hiyo iliyoweza kukusanya shilingi bilioni 3.2 na kuvuka malengo ya harambee hiyo kwa asilimia sita
 Rais Jakaya Kikwete, akimkabidhi picha ya kuchora Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya UNDI Consulting Group Limited, Bw Philip Makoka aliyoinunua kwa shilingi milioni 20 wakati wa Harambee ya kuchangia fedha programu ya Mkapa Fellows inayoendeshwa naTaasisi ya Mkapa HIV/AIDS iliyofanyika Dar es Salaam kwenye hoteli ya Kilimanjaro Hyatt  Regency jijini Dar es salaam. Kulia ni mchoraji wa picha hiyo, Bwana Muzu
 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akisindikizwa  na  Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi (kushoto)  na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mzee Benjamin William Mkapa baada ya kuwa mgeni rasmi katika harambee ya kuchangia Taasisi ya Mkapa HIV/AIDS foundation na kusaidia  kukusanya shilingi bilioni 3.2 nauvuka malengo ya harambee hiyo kwa asilimia sita.PICHA NA IKULU

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages