MTOTO WA MBUNGE SITTI MTEMVU AMSAIDIA SH. 500,000 MSICHANA HAPPINESS KAAYA MLEMAVU ANAYEISHI NDANI KWA MIAKA 22 - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

MTOTO WA MBUNGE SITTI MTEMVU AMSAIDIA SH. 500,000 MSICHANA HAPPINESS KAAYA MLEMAVU ANAYEISHI NDANI KWA MIAKA 22

MWANAFUNZI wa Chuo Kukuu cha North Texas cha Marekani, Sitti Mtemvu (kushoto), akitoa msaada wa sh. 500,000 kwa msichana Happines Kaaya (22), aliyezaliwa akiwa mlemavu, katika hafla iliyofanyika Machimbo, Temeke, Dar es Salaam juzi.

 Mamake Sitti, Mariam Mtemvu, ambaye ni mke wa Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu ampa pole Happiness.
 Sitti ambaye ni mtoto wa kwanza wa Mbunge wa Jimbo la Temeke, akimbusu Happiness baada ya kutoa msaada huo. Sitti pia ni  mmoja wa wakurugenzi wa Mtemvu Foundation
 Mmoja wa wapangaji wa nyumba anayoishi Happiness na mamake Khadija Msuya akielezea jinsi wanavyomsaidia msichana huyo mlemavu
Sitti akitoa msaada mwingine wa sh. 200,000 kwa mtu mwenye ulemavu, Nassoro Tayari mkazi wa Buza jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kununulia vipuri vya kutengenezea baiskeli yake.
Na Richard Mwaikenda

MWANAFUNZI wa Chuo Kukuu cha North Texas, Marekani, Sitti Mtemvu, ametoa msaada wa sh. 500,000 kwa msichana Happines Kaaya (22), aliyezaliwa akiwa mlemavu.

Msaada huo alikabidhi kwa mama mzazi wa Happiness, Khadija Msuya katika hafla iliyofanyika kwenye chumba  wanachoishi  eneo  la Machimbo, Temeke, Dar es Salaam juzi.

Siti ambaye pia ni Mkurugenzi wa  Mtemvu Foundation, alisema kuwa ameamua kutoa msaada huo baada ya kuguswa na taarifa za msichana huyo alizozisoma kwenye mafaili ya mfuko huo, zilizopo Temeke, Dar es Salaam.

"Taarifa za msichana huyu, zilinigusa mno kuliko wengine, kiasi cha kuamua kuanza kutoa msaada kwa Happiness aliyezaliwa akiwa mlemavu na analelewa mamake kwa shida,"alisema Siti.

Siti ambaye ni mtoto wa kwanza wa Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu, alisema kuwa fedha alizizitoa ni sehemu ya mapato yanayotokana na bajaji zake tatu zinazofanya biashara ya kubeba abiria jijini  Dar es Salaam.

Alisema kuwa Bajaji hizo alizinunua kutoka na na fedha alizolipwa baada ya kushiriki kwenye filamu moja nchini Marekani anakosoma.

"Sitoishia kutoa msaada kwa msichana huyo, bali nina imani Mungu akinijalia nitaendelea kutoa msaada kwa yatima na watu wengine wanaoishi kwenye mazingira magumu"alisema Siti.

Mama mzazi wa Happiness, Khadija, alishukuru kupata msaada huo kutoka kwa Sitti, ambao alidai utamsaidia sana kupunguza baadhi ya matatizo yanayomkabili.

Alisema kuwa mtoto huyo ambaye alimzaa akiwa na ulemavu, hana uwezo wa kutembea ambapo hata kula chakula ni vigumu inabidi alishwe na kumsaidia wakati wa kujisaidia.

Alidai kuwa Baba mzazi wa Happiness, Joel Kaaya  alimtelekeza yeye na mwanawe ambapo mpaka sasa haijulikani aliko.

Msuya alitoa wito kwa watanzania wengine kujitokeza kusaidia hata ikiwezekana kumnunulia happiness kiti cha magurudumu kitakachorahisisha kumpeleka Hospitali na hata kutoka nje kucheza na wasichana wenzie.

Pia siku hiyo, Siti alitoa msaada mwingine wa sh. 200,000 kwa mtu mwenye ulemavu, Nassoro Tayari mkazi wa Buza jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kununu vipuri vya kutengenezea baiskeli yake.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages