Matukio ya Msiba wa Marehemu Willy Edward, Mburahati Dar Es Salaam - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Matukio ya Msiba wa Marehemu Willy Edward, Mburahati Dar Es Salaam

 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Jambo Concepts Limited, inayochapisha gazeti la Jambo Leo na jarida la Jambo Brand Tanzania, Juma Pinto (kushoto) na Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Benny Kisaka (wa pili kushoto) wakiwa kwenye msiba wa aliyekuwa Mhariri Mkuu wa Jambo Leo, marehemu Willy Edward Ogunde ulioopo nyumbani kwa kaka wa marehemu Mburahati, Dar es Salaam leo asubuhi. Wiily amefariki ghafla leo alfajiri mjini Morogoro alikokuwa akihudhuria semina ya siku moja ya masuala ya Sensa. Kutoka kulia ni ndugu zake marehemu; Dennis Ongiri, Joseph Rabach na Julius Rabach.
 Waandishi wa habari wa gazeti la Jambo Leo na Jarida la Jambo Brand Tanzania wakishiriki kwenye msiba wa aliyekuwa Mhariri Mkuu wa gazeti la Jambo Leo, marehemu Willy Edward. Mwili wa marehemu Willy unasafirishwa mchana huu kutoka Morogoro kwenda kuhifadhiwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam. Taratibu za mazishi zinaendelea kuratibiwa kwa ushirikiano wa ndungu na viongozi wa Jambo Concepts, lakini kwa mujibu wa Kaka wa marehemu Rabach ni maazishi yatafanyika nyumbani kwao marehemu, mjini Mugumu Wilaya ya Serengeti, mkoani Mara. Siku ya mazishi itatangazwa baadaye.

   Mjane wa marehemu Willy Edward, Rehema, akiwa kwenye majonzi
 Mjane wa marehemu Willy Edward, Rehema akilia wakati wa msiba huo leo asubuhi
 Waombolezaji wakimfariji mjane wa marehemu Willy Edward, Rehema

Akina mama waombolezaji wakiwa kwenye msiba
 Mtangazaji wa TBC, Grace Kingarame akimfariji  mjane wa marehemu Willy Edward, Rehema.
 Mpiga picha wa TBC, Mary Hondo, akimfariji Rehema.
 Mtoto wa mwisho wa marehemu Willy Edward, Caren (2), akiwa na babake mkubwa, Dennis Rabach
 
Mtoto wa mwisho wa marehemu, Willy Edward, Caren akiwa katika msiba
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Jambo Concepts Limited, inayochapisha gazeti la Jambo Leo na jarida la Jambo Brand Tanzania, Juma Pinto akihojiwa na Grace Kingarame wa TBC katika msiba huo. (Picha zote na Richard Mwaikenda 'Kamnada wa Matukio')

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages