Epiq Bongo Star Search yamaliza kazi mkoani Dodoma - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Epiq Bongo Star Search yamaliza kazi mkoani Dodoma

Madam Ritah Paulsen akipokea mtoto kutoka kwa  mshiriki huyu aliyekuja nae katika shindano hilo kabla  kuanza kuimba.
Mkuu wa kitengo cha mawasiliano Zantel ambao ni wadhamini wakuu wa EBSS 2012  Awaichi Mawalla akichangia damu 

Na Mwandishi Wetu Dodoma
PAZIA la shindano la Epiq Bongo Star Search (EBSS) kwa mkoa wa Dodoma limefungwa rasmi huku vipaji kibao vikiwa vimejitokeza na kuwavutia majaji.

Kilichovutia zaidi ni washiriki wa miaka 16 ambao walionekana kuimba vema na kuwa kivutio hata kwa washiriki wenzao waliofurika katika ukumbi wa Royal Village.

Akizungumzia shindano hilo Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Benchmark Production inayoandaa shindano hilo Ritha Paulsen alisema kuwa amevutiwa na wingi wa washiriki mkoani hapa hasa idadi ya washiriki wasichana pia.

Alisema kuwa ikiwa ni mara ya kwanza kuruhusu washiriki wa miaka 16 kuingia katika usaili wa EBSS 2012 ameshuhudia hazina kubwa ya vipaji  vya washiriki wa umri huo.

Katika usaili huo kulikuwa na washiriki wa aina mbalimbali wakiwamo wanafunzi, wafanyabiashara ndogondogo, vijana wa mitaani na wadau wengineo wa muziki.

Kwa kuthamini umuhimu wa akina mama na watoto mshiriki aliefika kuonesha kipaji chake katika ukumbi huo alipewa nafasi ya kuimba ili aweze kuwahi kuondoka.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Zantel ambao ni wadhamini wakuu wa EBSS 2012  Awaichi Mawalla mbali na kuvutiwa na ushiriki wa vijana waliojitokeza pia alihamasisha upimaji wa damu kwa kuchangia damu kwa kituo cha damu mkoani Dodoma.

“ Kwa kupitia EBSS 2012 tunataka kuwafikia vijana sio tu katika muziki bali pia hata katika kuhamasisha masuala mbalimbali yahusuyo jamii kama vile hili la kuchangia damu na mengineo” alisema Awaichi.

Washindi watakaopatikana watatangazwa baadae katika vyombo vya habari. Baada ya Dodoma kwa sasa inafuata Zanzibar ijumaa ijayo katika eneo la Ngome Kongwe

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages