RAIS JAKAYA KIKWETE AZINDUA MRADI WA MAJI PAWAGA, UMEGHARAMIWA NA KANISA LA ANGLICAN KWA ZAIDI YA BILIONI MBILI - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

RAIS JAKAYA KIKWETE AZINDUA MRADI WA MAJI PAWAGA, UMEGHARAMIWA NA KANISA LA ANGLICAN KWA ZAIDI YA BILIONI MBILI

Rais Jakaya Kikwete akifungua maji ya bomba kuashiria uzinduzi rasmi wa mradi wa maji katika kijiji cha Itunundu kata ya Pawaga Iringa uliogharimiwa na kanisa la Anglican Dayosisi ya Luaha Mkoani Iringa kwa zaidi shilingi bilioni mbili, Huku wakuu wa kanisal hilo wakishuhudia, kutoka kulia ni Askofu mstaafu wa Dayosisi ya Luaha Dornald Mtetemela, Martha Mgomi Mratibu wa mradi huo na Askofu Joseph Mgomi wa Daayosisi ya Luaha. FULLSHANGWE ilikuwepo katika msafara huo na kukuletea taswira mbalimbali za kuwasili kwa Mh. Rais Jakaya Kikwete pamoja na shughuli yake ya kuzindua mradi wa maji katika kijiji cha Itunundu kata ya Pawaga mkoani Iringa.
Rais Jakaya Kikwete akimpongeza mama Agnes Msavi mara baada ya kumtwisha ndoo ya maji kuashiria ukombozi kwa mwanamke kutokana na kukamilika kwa mradi huo.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiripoti tukio hilo huko Pawaga Itunundu.
Rais Jakaya Kikwete akiwasili kijijini Itunundu Pawaga tayari kwa kuzindua mradi huo.
Vijana wa Kimasai wakicheza ngoa yao wakati wakimkaribisha Rais jakaya Kikwete kijijini hapo leo.
Warembo wa kimasia wakiwmlaki Rais Jakaya kikwete huku wakiwa wameshikilia bendera za taifa alipowasili katika kijiji cha Itunundu.
Umati wa wananchi ukimsubiri Rais Jakaya Kikwete katika kijiji cha Itunundu.
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Kamanda wa vijana mkoani Iringa Salim "Sas" Abri mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Nduli mjini Iringa.
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na kada wa Chama cha Mapinduzi Venance Mwamoto.
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Askofu wa Dayosisi ya Luaha Joseph Mgomi wakati alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Nduli mjini Iringa leo mchana, kushoto ni Askofu mstaafu wa Dayosisi ya Luaha Dornald Mtetemela.
Rais Jakaya Kikwete akiwatunza wasanii wa kikundi cha ngoma kilichokuwa kikitumbuiza wakati alipowasili mjini Iringa leo.
Rais Jakaya Kikwete akiongozana na Mkuu wa mkoa wa Iringa Dk. Christine Ishengoma kushoto mara baada ya kuwasili mjini Iringa leo, kulia ni Naibu Waziri wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Grayson Rwenge.
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Evarist Mangalla katika uwanja wa ndege wa Nduli.Picha Kwa Hisani ya Full Shangwe

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages