Rotary Club Tanzania kutumia dola za kimarekani zaidi ya Mil 1 kwa ajili ya kusambaza maji katika maeneo yenye uhaba wa maji - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Rotary Club Tanzania kutumia dola za kimarekani zaidi ya Mil 1 kwa ajili ya kusambaza maji katika maeneo yenye uhaba wa maji

Wakiwa katika picha ya pamoja.
 
Harry Mugo kutoka Rotary Club ya Nairobi North akizungumza katika mkutano huo.
Mwenyekiti wa Rotary Clabu Tanzania Harish Bhatt (kulia) akimkabidhi bendera ya Rotary, Harry Mugo kutoka Rotary Club ya Nairobi North.

KATIKA kukabiliana na tatizo la maji nchini RoratyClabu Tanzania inatarajia kutumia dola za kimarekani zaidi ya milioni moja mwaka ujao kwa ajili ya kutekeleza mradi wa tekinolojia ya kisasa ya kuchimba visima pamoja na kusambaza maji katika maeneo yenye uhaba.

Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa Rotary Clabu Tanzania Harish Bhatt, kwenye mkutano wa tatu wa mwaka uliofanyika jijini Dar es Salaam, ukiwa na lengo la kubadilishana uzoefu na kupanga mikakati ya mwaka ujao.

Aidha alisema, tayari mradi wa maji ulishaanza kwa kusambaza maji katika shule 20 za mkoa wa Dar es Salaam na kwamba ni matumaini yao kwa mwaka ujao wataenda kwenye maeneo yasio na maji kwa lengo la kuhakikisha tatizo linapungua kama si kuisha kabisa.

Alisema kwa sasa rotary clabu ina malizia mradi wa kujenga wadi ya watoto wanaosumbuliwa na magonjwa ya saratani katika hospitali ya taifa ya Muhimbili pamoja na miradi mingine ya kimaendeleo kote nchini.

Mradi wa maji kwa mwaka ujao ni makubaliano ya Rotary clubu zote za Afrika kuwa pamoja na miradi mingine ya maendeleo maji yatapewa kipaumbele cha kwanza.

"Maji imekuwa ni tatizo kubwa hivyo kupitia clabu zetu tutaandaa marathoni nyingine kwa lengo la kukusanya pesa kwa ajili ya mrdia mkubwa wa maji mwakani utao tumia tekinolojia ya kisasa mkutano huu ambao hufanyika mara moja tu mwaka unalengo la kujua ni wapi tumekosea pamoja na kubadilishna mawazo na kupanga mikakati yetu" alisema.

Akifungua mkutano huo Gavana Mteule kutoka nchi tano za Afrika Geeta Manek alishukuru Tanzania kwa kuendeleza amani nchini na kuwa na moyo wa kujitolea kwa ajili ya wengine tofauti na nchi nyingine.

Alisema rotary haina udini wala ukabila kila mwenye vigezo anaweza kujiunga kwa lengo la kusaidia watu wenye mahitaji mbalimbali ikiwa ni malengo makuu ya kuanzishwa kwa clabu hiyo kote duniani.

Gavana huyo mteule ambaye amesisitiza amani ncini anawakilisha nchi za Kenya, Uganda, Elitrea, Tanzania na Ethiopia.

Kwa upande wake Katibu wa Rotary Clabu Mkoa wa Rukwa Daniel Mtweve alishukuru watanzania kwa kuondoa dhana potofu ya kudhani rotary ipo kwa ajili wa wahindi peke yako badala yake wamejiunga kwa wengi.

Alisema kwa sasa mkoa wa Rukwa baadhi ya wakazi wameshafaidika na miradi yao inayoendelea ukiwemo ule wa kusaidia madawati kwa watoto wa shule.

Mkutano huo wa siku moja uliandaliwa na Rotary Club ya Dar es Salaam ambapo jumla ya wanachama 200 walishiriki kwa lengo la kubadilishana mawazo na uzoefu.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages