RAIS JAKAYA KIKWETE ASHIRIKI MATEMBEZI YA KUCHANGISHA FEDHA KUSAIDIA KINA MAMA WENYE MATATIZO YA FISTULA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

RAIS JAKAYA KIKWETE ASHIRIKI MATEMBEZI YA KUCHANGISHA FEDHA KUSAIDIA KINA MAMA WENYE MATATIZO YA FISTULA



Rais Jakaya Kikwete wa nne kutoka (kulia) akishiriki katika matembezi ya kuchangia shilingi Bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa jengo la akina mama wenye matatizo ya ugonjwa wa Fistula katika hospitali ya CCBRT leo asubuhi jijini Dar es salaam, matembezi hayo yameanzia katika hoteli ya Golden Tulip na kumalizika katika Hospitali ya CCBRT Mikocheni, matembezi hayo yameandaliwa kwa pamoja na kampuni ya Vodacom Tanzania, Vodafone pamoja na hospitali ya CCBRT Kampeni hiyo inajulikana kama (Finde your Moyo).
Rais Jakaya Kikwete, Katibu Mkuu wa Chadema, Willbroad Slaa na Mkurugenzi wa Huduma za Jamii wa CCBRT, Brenda Msangi  wakishiriki katika mazoezi  alipokuwa katika matembezi hayo leo.
Rene Meza Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania akitoa hotuba yake kabla ya kuanza kwa matembezi hayo leo asubuhi. Watu mbalimbali waliojitokeza katika matembezi hayo wakiwa katika hoteli ya Golden Tulip leo asubuhi.
Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya CCBRT Bw. Wilbroad Slaa akizungumza na Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba.
Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba akizungumza na Rene Meza Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania.
Wakiwa katika mzungumzo kabla ya kuanza kwa matembezi hayo kulia ni Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es salaam ya kipolizi Suleiman Kova, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Rugimbana na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Hadji Mponda.
Muandaaji wa Lukaza Blog, Josephat Lukaza nilikuwepo pia kwenye matembezi ya kuchangia ujenzi wa hospitali kwaajili ya wanawake wenye fistula ambayo yameandaliwa na Vodacom Tanzania wakishirikiana na Vodafone Foundation
Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu Salva Rweyemamu akijadili jambo na Meneja Udhamini na Matukio wa Vodacom Tanzania Rukia Mtingwa. Watu mbalimbali walioshiriki katika matembezi hayo
Kulia ni Grace Lyon wa Vodacom Tanzania, Meneja wa Vodacom Foundation Yesaya Mwakifulefule na Matina Nkurlu Meneja wa kitengo cha habari za Mtandao Vodacom Tanzania.
Wadau wangu wakubwa kulia ni Bw. Philip Seyayi aka (Shvangirai) kutoka JWT na Ofisa Udhamini wa Vodacom Tanzania Ibrahim Kaude wakipata viroba vyao! Ah ni utani tu jamani hii ni Juice.

Mazoezi yanaendelea.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages