WAKAZI WA KANDA YA ZIWA WAENDELEA KUJIZOLEA ZAWADI ZA MZUKA WA SOKA NA COKA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

WAKAZI WA KANDA YA ZIWA WAENDELEA KUJIZOLEA ZAWADI ZA MZUKA WA SOKA NA COKA

 Meneja Masoko na Mauzo na Masoko wa Coca-Cola Nyanza, akiongea na waandishi wa habari.
 Washindi mbalimbali wakikabidhiwa zawadi zao.
Baadhi ya washindi wakifurahia zawadi walizojishindia.
---
Promosheni ya Mzuka wa Soka na Coka ya kampuni ya Coca-Cola Nyanza Bottlers ya jijini Mwanza inazidi kuwezesha wateja wa soda kujishindia zawadi ambapo wiki hii wateja 11 wamekabidhiwa pikipiki na wengine 4 wamekabidhiwa luninga bapa za kisasa.

Akiongea katika hafla ya kukabidhi zawadi kwa washindi,Meneja Masoko na Mauzo wa Nyanza Bottlers,Samwel Makenge ,alisema kumekuwa na ongezeko la washindi ,na kampuni inayo furaha kuona wateja wake wanaendelea kushiriki katika promosheni hii na kuweza kujishindia zawadi mbalimbali.

“Zipo zawadi nyingi zimeandaliwa kwa ajili ya wateja wetu zikiwemo pikipiki,luninga bapa za kisasa,fedha taslimu kuanzia 5,000 hadi 100,000/-na soda za bure, tunatoa wito waendelee kushiriki waweze kujishindia”,Alisema Makenge.

Washindi wapatao 15 ambao walikabidhiwa zawadi zao za Pikipiki naLuninga katika hafla hiyo iliyofanyika katika kiwanda cha Nyanza, waliishukuru kampuni ya Coca-Cola kwa kubuni promosheni zenye mwelekeo wa kuwakwamua wateja wake kiuchumi.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages