Sunday, February 19, 2012

AMINI MWINYIMKUU ATIMULIWA THT

AMINI MWINYIMKUU - BONGO FLAVA ARTIST

MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Amini, amesema kuwa ametimuliwa rasmi Tanzania House of Talents ‘THT’, lakini anahisi kama ameonewa kutokana na mabavu yaliyotumika. Vyanzo vya habari vililipoti kuwa msanii huyo anajandiliwa na uongozi, lakini sasa taarifa iliyopatikana kutoka kwa muhusika zinadai tayari ameshawekwa pembeni. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, huku akitokwa na machozi alisema kuwa uongozi haujatenda haki kwani kosa la kinidhamu alilofanya walipaswa kukaa naye na kuzungumza lakini wameamua kumfukuza kitu ambacho anahisi ameonewa. “Mimi sioni kama kuwa wema ndani ya THT, ila nachoweza kusema kwamba naenda kufanya muziki wangu na mungu atanijalia tu kwa sababu kila kitu ni mipango,” Amini  alipigilia msumali wa mwisho.

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
Join me on Facebook Follow me on Twitter Find me on Youtube